Yanga - Local

Kamwe awatuliza mashabiki Yanga

Joel JJ By Joel JJ
β€’
17 Apr 2023
Kamwe awatuliza mashabiki Yanga

Meneja wa Habari na Mawasiliano klabu ya Yanga Ali Kamwe amesema licha ya kupoteza mchezo dhidi ya Simba jana, malengo yao yamebaki katika kuhakikisha wanatwaa ubingwa wa ligi kuu

Kamwe amesema ni kawaida kwa timu yoyote kupitia nyakati za kupoteza mchezo lakini jambo muhimu ni kuhakikisha hawatoki katika malengo yao makuu ambayo ni kushinda makombe

"Tukiwa na Unbeaten 49, Tukapoteza dhidi ya Ihefu, Tena ikiwa kwenye nafasi ya mwisho kwenye msimamo. Ilituumiza. Lakini nini kilifata baada ya pale? Tulishinda mechi 13 za Ligi mfululizo. Tukafuzu Robo Fainali ya CAF. Na kama haitoshi, Tukafuzu Nusu Fainali ya Kombe la Shirikisho la Azam"

"Unafikiri hayo yote yalitokea kwa bahati mbaya? Si kweli. Siri nyuma yake ni Kutopoteza malengo. MALENGO yetu ni Nini msimu huu? kubeba makombe. Kila Mwanayanga anataka kuiona Timu yake ikibeba Kombe la Ligi, Kombe la Shirikisho la Azam na Ubingwa wa Afrika"

"Tunaimaliza April. Mwezi unaofata, utakuwa mwezi wa mapigano makubwa katika kuyafikia malengo yetu. Vyakula vyote vizuri bado viko juu ya meza yetu. Tutulie na Tushikane Wananchi"

"Kupoteza pambano sio kupoteza vita. Jana Tumepoteza pointi 3, hatujapoteza Malengo yetu ya Ubingwa Msimu huu," aliandika Kamwe kwenye ukurasa wake wa mtandao wa kijamii"

Licha ya kipigo kutoka kwa watani zao Simba hapo jana, Yanga imeendelea kubaki kileleni mwa msimamo wa ligi ya NBC ikiwa na alama 68 huku Simba ikipunguza gap la pointi kutoka nane na kubaki tano baada ya kufikisha alama 63

Kila timu imesalia na mechi nne kuhitimisha msimu Yanga ikihitaji alama nane kutetea ubingwa

More Stories

Barcelona yaendeleza dozi La Liga, yaipiga Racing Santander 7-2
Barcelona yaendeleza dozi La Liga, yaipiga Racing Santander 7-2
1h ago
READ MORE β†’
Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
11h ago
READ MORE β†’
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
11h ago
READ MORE β†’
Highlights : Azam Fc 0-2 Simba
Highlights : Azam Fc 0-2 Simba
11h ago
READ MORE β†’
Mizizima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
Mizizima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
15h ago
READ MORE β†’
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
18h ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
19h ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
20h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
20h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
21h ago
READ MORE β†’