Ukame wa mabao waikumba Barcelona

Joel JJ By Joel JJ β€’ 17th April 2023


Ukame wa mabao waikumba Barcelona

Barcelona walishindwa kufunga bao kwa mechi ya tatu mfululizo baada ya kutoka sare tasa ya La Liga kwenye uwanja wa Getafe Jumapili jioni

Raphinha na Alejandro Balde wote waligonga nguzo kwa mfululizo katika kipindi cha kwanza na Barca hawakuweza kupata matokeo ya ushindi

Sare hiyo ni ya pili baada ya sare nyingine dhidi ya Girona Jumatatu iliyopita pia wakitoka kupoteza kwa mabao 4-0 katika Copa del Rey dhidi ya Real Madrid

Licha ya mapambano yao ya kufunga mabao, Barca wanaongoza kwa pointi 11 dhidi ya Madrid huku zikiwa zimesalia mechi tisa za ligi.


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.