Barcelona walishindwa kufunga bao kwa mechi ya tatu mfululizo baada ya kutoka sare tasa ya La Liga kwenye uwanja wa Getafe Jumapili jioni
Raphinha na Alejandro Balde wote waligonga nguzo kwa mfululizo katika kipindi cha kwanza na Barca hawakuweza kupata matokeo ya ushindi
Sare hiyo ni ya pili baada ya sare nyingine dhidi ya Girona Jumatatu iliyopita pia wakitoka kupoteza kwa mabao 4-0 katika Copa del Rey dhidi ya Real Madrid
Licha ya mapambano yao ya kufunga mabao, Barca wanaongoza kwa pointi 11 dhidi ya Madrid huku zikiwa zimesalia mechi tisa za ligi.



