Mfungaji bora wa michuano ya Kombe la Mapinduzi 2023, Francy Kazadi anayekipiga Singida Big Stars amekwama kabisa kwenye Ligi Kuu Bara akishindwa kufunga bao lolote hadi sasa
Lakini kocha mkuu wa timu hiyo, Hans Pluijm amefichua kinachokwamisha nyota huyo Mkongoman
Pluijm alisema siri kubwa inayomkwamisha Kazadi aliyemaliza Mapinduzi kwa kufunga mabao sita ni kushindwa kuzoea kwa haraka mazingira, huku akimsifia ni mchezaji mzuri na kumtabiria kuja kufunika atakapoizoea Ligi Kuu
"Kuzoea mazingira kwa haraka kwake ndio changamoto kubwa, unajua ametoka sehemu ambayo timu nzuri na alikuwa anacheza kwenye viwanja vizuri kwahiyo hapa inampa tabu kidogo"
"Kama mchezaji anatakiwa azoee mazingira kwa haraka ili aweze kufanya kazi yake, nina imani nae kwamba ni mchezaji ambaye anajituma na yupo tayari kuipambania timu," alisema Pluijm
Kazadi alijiunga na Singida BS kwenye dirisha dogo la msimu huu baada ya kumaliza mkataba aliokuwa nao na El Masry ya Misri, huku akiwa mzoefu wa soka la Arabuni akiwahi kuichezea Mohammedia, Wydad Casablanca, El Masry na Gaish
Kwenye michuano ya Mapinduzi ambao Mlandege ilibeba ubingwa kwa kuifunga Singida BS, mshambuliaji huyo alifunga mabao sita



