Klabu ya Bayern Munich imempiga faini, Sadio Mane na huenda wakafungua milango kwa nyota huyo kuondoka kipindi cha majira ya joto kwa kitendo chake cha kumpiga ngumi mchezaji mwenzake, Leroy Sane baada ya mechi yao na Man City
Tukio la Mane kumpiga Leroy Sane limetokea baada ya miamba hiyo ya Ujerumani kupokea kichapo cha goli 3-0 dhidi ya Manchester City Jumanne iliyopita
Sane alionekana kuumia sehemu ya lipsi za mdomo kufuati ngumi hiyo
Mane alisimamishwa kwa muda na kukosa mechi ya Bundesliga dhidi ya Hoffenheim siku ya Jumamosi huku akilimwa faini
Inaripotiwa kuwa mchezaji huyo wa Senegal amepigwa faini kubwa mno kuwahi kutokea kwenye historia ya klabu ya Bayern Munich ipatayo zaidi ya pauni 260,000
Tayari amerejeshwa kikosini kwa ajili ya maandalizi ya mchezo wa marudiano ligi ya mabingwa dhidi ya Manchester ambao utapigwa Jumatano



