Bayern kumuweka sokoni Mane

Joel JJ By Joel JJ β€’ 18th April 2023


Bayern kumuweka sokoni Mane

Klabu ya Bayern Munich imempiga faini, Sadio Mane na huenda wakafungua milango kwa nyota huyo kuondoka kipindi cha majira ya joto kwa kitendo chake cha kumpiga ngumi mchezaji mwenzake, Leroy Sane baada ya mechi yao na Man City

Tukio la Mane kumpiga Leroy Sane limetokea baada ya miamba hiyo ya Ujerumani kupokea kichapo cha goli 3-0 dhidi ya Manchester City Jumanne iliyopita

Sane alionekana kuumia sehemu ya lipsi za mdomo kufuati ngumi hiyo

Mane alisimamishwa kwa muda na kukosa mechi ya Bundesliga dhidi ya Hoffenheim siku ya Jumamosi huku akilimwa faini 

Inaripotiwa kuwa mchezaji huyo wa Senegal amepigwa faini kubwa mno kuwahi kutokea kwenye historia ya klabu ya Bayern Munich ipatayo zaidi ya pauni 260,000

Tayari amerejeshwa kikosini kwa ajili ya maandalizi ya mchezo wa marudiano ligi ya mabingwa dhidi ya Manchester ambao utapigwa Jumatano


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.