Ni Jumanne ya Ligi ya mabingwa barani Ulaya ambapo Chelsea inakabiliwa na kibarua kigumu cha kupindua meza kufuatia kipigo cha 2-0 kwenye mchezo wa mkondo wa kwanza dhidi ya Real Madrid katika Uwanja wa Stamford Bridge
Ni mchezo unaozikutanisha timu mbili ambazo zimeshinda ubingwa wa Ulaya kwa kipindi cha miaka miwili iliyopita, The Blues wakitwaa UCL mnamo 2021 huku Real Madrid wakitwaa kombe hilo mwaka jana 2022
Chelsea chini ya kocha wa muda Frank Lampard, watahitaji kufanya kazi ya ziada kuweza kuwaondosha mabingwa hao wa kihistoria katika ligi ya mabingwa
Chelsea hawana mwenendo mzuri wakikosa ushindi katika mechi tano zilizopita katika mashindano yote
Mechi nyingine itakayopigwa leo, itahusishwa derby ya Italia ambapo mabingwa watetezi wa Serie A, AC Milan wakiwa ugenini dhidi ya mabingwa watarajiwa wa Serie A, Napoli katika mchezo mwingine wa raundi ya pili ya hatua ya robo fainali ya UCL
AC Milan ilishinda bao 1-0 katika mchezo wa mkondo wa kwanza, itakuwa na kibarua cha kulinda ushindi wake katika dimba la Diego Maradona