Simba - Local

Simba yaanza mawindo ya Wydad Athletic

Joel JJ By Joel JJ
β€’
18 Apr 2023
Simba yaanza mawindo ya Wydad Athletic

Meneja wa Habari na Mawasiliano klabu ya Simba Ahmed Ally amesema maandalizi kuelea mechi dhidi ya Wydad Athletic yameanza leo kikosi cha Simba kikiingia kambini kwa ajili ya mchezo huo wa robo fainali ligi ya mabingwa barani Afrika

Mchezo utapigwa Jumamosi, April 22 saa 10 jioni katika uwanja wa Benjamin Mkapa

Akizungumza katika Mkutano na Wanahabari kuelekea mchezo huo, Ahmed alisema Simba itaanza kujifua Mo Simba Arena leo saa 10 jioni

"Kikosi kimeingia kambini kwa ajili ya maandalizi ya kuikabili Wydad Athletic siku ya Jumamosi, timu imeingia kambini saa 3 asubuhi. Jioni Simba itaendelea na mazoezi Mo Simba Arena"

"Wachezaji Sadio Kanoute aliyekuwa akisumbuliwa na majeraha ya nyonga na Aishi Manula wataripoti kambini kwa ajili ya kufanyiwa tathmini ya majeraha yao na madaktari watatoa mapendekezo yao iwapo waungene na wenzao kambini au bado wanahitaji muda zaidi wa matibabu"

"Augustinr Okrah amepona alirejea mazoezini wiki iliyopita lakini hakuwa fit kuweza kutumika katika michezo iliyopita," alisema Ahmed

Ahmed amesema klabu ya Wydad Athletic itawasili nchini kesho Jumatano pamoja na waamuzi wote wa mchezo huo ambao wanatoka nchi za Senegal na Ivory Coast

Pia kutakuwa na waamuzi wa VAR kwani kuanzia hatua ya robo fainali VAR inatumika

Mechi za robo fainali zitapigwa kwa usaidizi wa VAR waamuzi watawasili Jumatano

Ahmed ametaja viingilio vya mchezo huo; VIP A Tsh 30,000/-, VIP B Tsh 20,000/-, VIP C 10,000/- na Mzunguuko ni Tsh 5,000/-

Pia kuna Mnyama Package maalum kwa ajili ya marafiki wanaonunua tiketi pamoja na Simba Executive ticket inayopatikana kwa Tsh 20,000/-

Platinum pia zipo kwa gharama ya Tsh 150,000/-

More Stories

Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
24m ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
1h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
1h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
2h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
3h ago
READ MORE β†’
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
3h ago
READ MORE β†’
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
16h ago
READ MORE β†’
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
16h ago
READ MORE β†’
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
17h ago
READ MORE β†’
Clement Mzize arejea rasmi kikosini baada ya miezi sita nje kwa majeraha
Clement Mzize arejea rasmi kikosini baada ya miezi sita nje kwa majeraha
22h ago
READ MORE β†’