Klabu ya Simba leo imezindua hamasa kuelekea mchezo wa mkondo wa kwanza robo fainali ya michuano ya ligi ya mabingwa barani Afrika dhidi ya Wydad Athletic
Mchezo huo utapigwa Jumamosi, April 22 katika uwanja wa Benjamin Mkapa, saa 10 jioni
Simba imesafiri mpaka Chalinze mkoani Pwani kuzindua hamasa katika kuhakikisha mashabiki wake wanajitokeza kwa wingi katika mchezo huo ambao Simba inahitaji kutumia vyema uwanja wa nyumbani kwa kuibuka na ushindi











