Simba yazindua hamasa Chalinze

Joel JJ By Joel JJ β€’ 19th April 2023


Simba yazindua hamasa Chalinze

Klabu ya Simba leo imezindua hamasa kuelekea mchezo wa mkondo wa kwanza robo fainali ya michuano ya ligi ya mabingwa barani Afrika dhidi ya Wydad Athletic

Mchezo huo utapigwa Jumamosi, April 22 katika uwanja wa Benjamin Mkapa, saa 10 jioni

Simba imesafiri mpaka Chalinze mkoani Pwani kuzindua hamasa katika kuhakikisha mashabiki wake wanajitokeza kwa wingi katika mchezo huo ambao Simba inahitaji kutumia vyema uwanja wa nyumbani kwa kuibuka na ushindi


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.