Mwaka mmoja uliopita Manchester City walipata kichapo cha kuhuzunisha zaidi Ulaya katika historia yao dhidi ya Real Madrid, lakini sasa wana nafasi ya kulipiza kisasi
Kwa msimu wa pili mfululizo City na Real zimepangwa katika nusu fainali ya Ligi ya Mabingwa
Mwaka jana City waliingia dakika ya mwisho ya mechi ya marudiano kwenye Uwanja wa Bernabeu wakihitaji tu kutoruhusu mabao mawili, lakini walifanya hivyo kwa mtindo wa kushangaza
Wakiwa ameshinda mechi ya mkondo wa kwanza 4-3 kwenye Uwanja wa Etihad, Riyad Mahrez aliipatia City uongozi wa jumla wa 5-3. Lakini Rodrygo aliyetokea benchi alifunga bao katika dakika ya 90 na 91
Karim Benzema akafunga bao la ushindi katika muda wa ziada kwa mkwaju wa penalti na kufanikiwa kuibuka na ushindi wa jumla wa 6-5 - na vijana wa Carlo Ancelotti wakaenda kuwashinda Liverpool kwenye fainali
Lakini kuna hisia halisi kwamba mambo yanaweza kuwa tofauti mwaka huu baada ya ushindi wa jumla wa 4-1 wa City dhidi ya Bayern Munich na kutinga nusu fainali ya tatu mfululizo - haswa wakiwa na mshambuliaji Erling Haaland mwenye mabao 48 katika safu yao.



