Manchester United - Sevilla - International

Ten Hag akubali, kuna tatizo Man United

Joel JJ By Joel JJ
β€’
21 Apr 2023
Ten Hag akubali, kuna tatizo Man United

Safu ya ulinzi ya Manchester United imeendelea kuonyesha udhaifu mkubwa katika jitihada zao za kujijenga upya kufuatia makosa mengi katika mchezo wa mkondo wa pili robo fainali ya ligi ya Europa dhidi ya Sevilla

Man United ilitolewa kwenye mashindano hayo Alhamisi usiku baada ya Sevilla kuwacharaza 3-0 na kuwaondosha kwa jumla ya mabao 5-2

Baada ya kuongoza kwa mabao 2-0 kabla ya mabao mawili ya kujifunga wenyewe mwishoni mwa mechi ya kwanza, Man United walikuwa na matumaini kwamba wangeweza kufika nusu fainali nyingine baada ya kushinda Kombe la Carabao na kutinga nusu fainali ya Kombe la FA

Lakini haikuwa hivyo, kwani makosa yao yaliwagharimu huku Youssef En-Nesyri na mchezaji wa zamani wa Nottingham Forest Loic Bade wakifunga mabao yaliyoipeleka Sevilla nusu fainali.

Baada ya kipigo hicho, mkufunzi wa Manchester United Erik ten Hag amekiri kuwa ipo changamoto katika safu yake ya ulinzi na kwa sasa ni lazima wakubali ili kupata ufumbuzi wa changamoto hiyo

More Stories

Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
26m ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
1h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
1h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
2h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
3h ago
READ MORE β†’
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
3h ago
READ MORE β†’
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
16h ago
READ MORE β†’
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
16h ago
READ MORE β†’
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
17h ago
READ MORE β†’
Clement Mzize arejea rasmi kikosini baada ya miezi sita nje kwa majeraha
Clement Mzize arejea rasmi kikosini baada ya miezi sita nje kwa majeraha
22h ago
READ MORE β†’