Bingwa mtetezi amepigika mbele ya Simba! Ndio ushindi wa bao 1-0 umeiweka Simba kifua mbele kuelekea mchezo wa marudiano robo fainali michuano ya ligi ya mabingwa barani Afrika dhidi ya Wydad Athletic
Jean Baleke ameendeleza kasi yake ya kuzifumania nyavu akifunga bao lake la nne katika michuano hiyo leo
Kazi nzuri kutoka kwa Kibu Denis kwenye dakika ya 41 ilimaliziwa vyema na Baleke aliyewazidi ujanja walinzi wa Wydad
Kipindi cha kwanza Simba ilicheza kwa tahadhari kubwa lakini kipindi cha pili iliongeza kasi na pengine ilistahili kufunga mabao zaidi Kibu Denis, Chama wakikosa nafasi
Ushindi wa nyumbani ni muhimu, vijana wa Robertinho Oliveira wanahitaji kwenda Morocco kwenda kulinda ushindi huo ili kukata tiketi ya kutinga nusu fainali


