Licha ya kupoteza mchezo dhidi ya Kitayose Fc, Timu ya JKT Tanzania imefanikiwa kurejea Ligi Kuu ya NBC baada ya kunufaika na matokeo ya sare ya bao 1-1 ambayo Pamba Fc waliyapa dhidi ya Mbuni Fc
JKT Tanzania imerejea Ligi Kuu ikiwa na michezo mitatu mkononi ikiwa imefikisha alama pointi 62 kileleni mwa ligi ya Championship
Vita imebaki kwa Kitayosce na Pamba kusaka mmoja wapo wa kuungana na Maafande hao kupanda moja kwa moja
Kitayoce wanashaika nafasi ya pili wakiwa na alama 53, huku Pamba wakiwa nafasi ya tatu na alama 52, timu zote zimebakiza mechi tatu kuhitimisha msimu



