JKT Tanzania yarudi Ligi Kuu

Joel JJ By Joel JJ β€’ 23rd April 2023


JKT Tanzania yarudi Ligi Kuu

Licha ya kupoteza mchezo dhidi ya Kitayose Fc, Timu ya JKT Tanzania imefanikiwa kurejea Ligi Kuu ya NBC baada ya kunufaika na matokeo ya sare ya bao 1-1 ambayo Pamba Fc waliyapa dhidi ya Mbuni Fc

JKT Tanzania imerejea Ligi Kuu ikiwa na michezo mitatu mkononi ikiwa imefikisha alama pointi 62 kileleni mwa ligi ya Championship

Vita imebaki kwa Kitayosce na Pamba kusaka mmoja wapo wa kuungana na Maafande hao kupanda moja kwa moja

Kitayoce wanashaika nafasi ya pili wakiwa na alama 53, huku Pamba wakiwa nafasi ya tatu na alama 52, timu zote zimebakiza mechi tatu kuhitimisha msimu


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.