Yanga imejiweka katika nafasi nzuri ya kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika baada ya ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Rivers United
Mabao mawili ya Fiston Mayele kutoka kwa assist mbili za Bakari Nondo Mwamnyeto yameacha kilio huko Nigeria
Wananchi walisema wanakwenda kulipa kisasi Nigeria, wamefanikiwa! kwani mabao mawili ambayo Rivers United waliifunga Yanga kwenye michuano ya ligi ya mabingwa mwaka 2021 yote yamelipwa!
Ni ushindi muhimu kwa Yanga ambao sasa unawafanya wahitaji sare au ushindi katika mchezo wa marudio utakaopigwa uwanja wa Benjamin Mkapa April 30





