Bao la Ferran Torres mwishoni mwa kipindi cha kwanza lilitosha kuipa Barcelona ushindi muhimu wa bao 1-0 dhidi ya Atletico Madrid katika harakati zao za kuwania ubingwa wa La Liga
Fowadi huyo wa zamani wa Manchester City alipokea pasi kutoka kwa Raphinha kutoka upande wa kushoto na akapiga shuti la chinichini lililomshinda Jan Oblak.
Atletico walitengeneza nafasi kadhaa kwenye kipindi cha kwanza Antoine Griezmann akikaribia kuwaadhibu waajiri wake hao wa zamani
Katika kipindi cha pili chenye burudani, pande zote mbili zilipata nafasi nyingi, lakini hakuna bao lililofungwa
Ushindi huo unaifanya Barcelona kufikisha pointi 11 mbele ya Real Madrid kileleni mwa La Liga, huku Atletico wakiwa nyuma kwa pointi tano dhidi ya wapinzani wao wa jiji hilo katika nafasi ya tatu



