Jana Real Madrid walipata kipigo kikali cha mabao 4-2 kutoka kwa Girona kwenye Uwanja wa Estadi Montilivi licha ya mabao ya kufarijiwa na Vinicius Junior na Lucas Vazquez
Girona walipata ushindi kupitia kwa mabao manne ya kushangaza kutoka kwa fowadi wa Argentina Valentin Castellanos
Real Madrid wanapigania kupata nafasi ya pili kwenye LaLiga Santander, huku Barcelona wakinyanyuka kuelekea taji hilo baada ya vijana wa Xavi kushinda 1-0 dhidi ya Atletico Madrid Jumapili.
Matokeo haya yanamaanisha kuwa Real Madrid wanasalia pointi 11 nyuma ya Barcelona ambao wako hatua moja karibu na kunyanyua taji la LaLiga Santander watakapomenyana na Rayo Vallecano Jumatano jioni