Kagera Sugar - Local

Afya ya beki aliyezimia Kagera Sugar yaimarika

Joel JJ By Joel JJ
β€’
27 Apr 2023
Afya ya beki aliyezimia Kagera Sugar yaimarika

Daktari wa Kagera Sugar, Abel Shindika amesema mlinzi Datius Peter ambaye alikumbwa na changamoto ya kuzimia katika mchezo wa ligi kuu dhidi ya Mbeya City, hakupata tatizo kubwa

Datius alizimia ghafla uwanjani baada ya kugongana na mshambuliaji wa Mbeya City, Sixtus Sabilo dakika ya 38 wakati wa mchezo wa Ligi Kuu Bara uliopigwa Aprili 23 kwenye Uwanja wa Kaitaba na wenyeji kushinda bao 1-0

Shindika amesema nyota huyo alipata mshtuko baada ya kugongwa sehemu ya goti lake kwa nyuma hivyo kumsababishia kupoteza fahamu ila baada ya kufanyiwa vipimo amegundulika hana tatizo lolote

"Tulimpima pale pale uwanjani lakini baada ya hapo tukampeleka hospitali ya karibu kwa ajili ya matibabu zaidi na tukagundua alipata mshtuko mdogo tu ambao hauna madhara yoyote hivyo anaendelea vizuri kwa sasa," alisema

Datius amesema lilikuwa jambo la kushtua katika maisha yake kwa sababu hali kama hiyo hajawahi kukutana nayo tangu ameanza mpira, hivyo anashukuru kwa sapoti kubwa ambayo wachezaji wenzake waliionyesha

"Nakumbuka nilizinduka hospitalini na baada tu ya hapo kitu cha kwanza niliuliza vipi matokeo, nikaambiwa tumeshinda basi kuanzia pale nikazidi kupata nguvu mwilini na nashukuru hadi sasa naendelea vizuri," alisema

More Stories

Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
9h ago
READ MORE β†’
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
9h ago
READ MORE β†’
Highlights : Azam Fc 0-2 Simba
Highlights : Azam Fc 0-2 Simba
9h ago
READ MORE β†’
Mizizima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
Mizizima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
13h ago
READ MORE β†’
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
16h ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
17h ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
17h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
18h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
19h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
20h ago
READ MORE β†’