Frank Lampard ataendelea kuwa meneja wa muda wa Chelsea hadi mwisho wa msimu huu, kulingana na Sky Sports
Klabu hiyo ilimweka Lampard usukani hadi majira ya joto mnamo Aprili 6 na hilo litabaki hivyo licha ya kuendelea kuwa na mfululizo wa matokeo mabaya
Mchakato wa klabu kupata meneja mpya wa kudumu bado unaendelea huku Mauricio Pochettino akiwa anaongoza na pengine atakabidhiwa majukumu mwishoni mwa msimu.
Wiki ijayo, Chelsea inatarajiwa kumtangaza kocha atakayechukua mikoba ya LampardΒ