Transfer - International

Tetesi za soka Ulaya, Ijumaa April 28 2023

Joel JJ By Joel JJ
β€’
28 Apr 2023
Tetesi za soka Ulaya, Ijumaa April 28 2023

Maafisa wa Real Madrid watasafiri hadi Ujerumani wiki hii katika jitihada za kumshawishi kiungo wa kati wa Borussia Dortmund na Uingereza Jude Bellingham, 19, kujiunga na klabu hiyo ya Uhispania msimu huu wa joto. (Marca kwa Kihispania)

Kiungo wa kati wa West Ham na England Declan Rice, 24, yuko kileleni mwa orodha ya wachezaji wanaolengwa na Arsenal msimu huu wa joto. (Telegraph - usajili unahitajika)

Kiungo wa kati wa Manchester United na Brazil Casemiro, 31, ananyatiwa na Thomas Tuchel katika klabu ya Bayern Munich msimu wa joto. (Kicker - kwa Kijerumani)

Mkufunzi wa Bayern Thomas Tuchel pia anataka kuungana tena na kiungo wa kati wa Chelsea na Croatia Mateo Kovacic, 28. (Sport1 - kwa Kijerumani)

Bayern, hata hivyo, hawana nia ya kumuuza kiungo wa kati wa Uholanzi Ryan Gravenberch mwenye umri wa miaka 20 msimu huu, licha ya vilabu vya Liverpool, Manchester United na Arsenal kuonyesha nia ya kutaka kumsajili. (CaughtOffside)

Mkufunzi wa zamani wa Bayern Munich Julian Nagelsmann yuko kileleni mwa orodha ya wachezaji wanne walioteuliwa kuwa mkufunzi mtarajiwa wa Tottenham Hotspur lakini Mjerumani huyo, 35, anaweza kuwa ghali sana kwa wachezaji hao wa London. (Telegraph - usajili unahitajika)

Aston Villa wanapania kumnunua mshambuliaji wa Brentford na England Ivan Toney, 27. (Football Insider)

Mshambulizi wa Ureno Joao Felix hatarejea Atletico Madrid msimu wa joto, huku mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 23 akitarajiwa kuongeza mkataba wake wa mkopo Chelsea. (Sun)

AC Milan wanafuatilia hali ya winga wa Arsenal Muingereza Reiss Nelson, 23, ambaye bado hajasaini mkataba mpya na The Gunners. (Calciomercato kupitia Football Italia - kwa Kiitaliano)

AC Milan pia wanavutiwa na kiungo wa kati wa Chelsea na Uingereza Ruben Loftus-Cheek, 27. (90min)

Manchester United wanatayarisha ofa ya kumnunua beki wa kulia wa Monaco Mbrazil Vanderson, 21, lakini huenda wakakabiliwa na ushindani kutoka kwa vilabu vingine kadhaa vya Ligi Kuu ya Uingereza. (RMC Sport kupitia Sun)

BBC

More Stories

Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
5h ago
READ MORE β†’
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
5h ago
READ MORE β†’
Highlights : Azam Fc 0-2 Simba
Highlights : Azam Fc 0-2 Simba
5h ago
READ MORE β†’
Mizizima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
Mizizima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
9h ago
READ MORE β†’
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
12h ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
13h ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
13h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
14h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
15h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
16h ago
READ MORE β†’