Beki wa Manchester City na England Kyle Walker, 32, anataka kusalia katika klabu hiyo licha ya muda wake mdogo wa kucheza msimu huu na Aston Villa na AC Milan wakimtaka (Star)
Newcastle na Manchester City wamejiondoa kwenye kinyang'anyiro cha kumsajili Mason Mount wa Chelsea , huku kiungo huyo wa kati wa Uingereza mwenye umri wa miaka 24 akitarajiwa kuondoka Stamford Bridge msimu huu wa joto. (Football Insider)
Arsenal bado wana nia ya kumsajili Mount msimu huu wa joto jambo ambalo linaweza kumaanisha The Gunners kusitisha nia yao ya kumsajili kiungo wa kati wa West Ham na England Declan Rice, 24.(Mail)
Bayern Munich wanavutiwa na mshambuliaji wa Aston Villa na England Ollie Watkins, 27, kama mbadala wa mshambuliaji wa Tottenham na Uingereza Harry Kane, 29 (Mirror)
Arsenal itasikiliza ofa kwa kiungo Granit Xhaka, 30, mlinzi Kieran Tierney, 25, na mshambuliaji Folarin Balogun mwenye umri wa miaka 21 ili kufadhili usajili wa kikosi kikali kwa lengo la kurejea Ligi ya Mabingwa. (Mirror)
Aston Villa wapo mstari wa mbele kumsajili nahodha wa Feyenoord Orkun Kokcu msimu huu wa joto, huku vilabu vingine vitano vya Ligi Kuu pia vikiwa vinamtaka kiungo huyo wa Uturuki mwenye umri wa miaka 22. (Mirror)
Inter Milan wanapanga kumnunua beki wa kati wa Fulham Tosin Adarabioyo, 25, ambaye amesalia na zaidi ya mwaka mmoja katika mkataba wake Craven Cottage. (Sky Sports)
Tottenham na AC Milan wanawania saini ya winga wa Newcastle Allan Saint-Maximin lakini Magpies wanataka ada ya £50m kwa mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 26. (Mirror)
Harry Maguire, 30, anahofia kwamba atalazimika kuondoka Manchester United msimu huu wa joto huku mlinzi huyo akihofia kupoteza nafasi yake katika kikosi cha England kabla ya Euro 2024. (Mail)
Arsenal wana nia ya kumnunua beki wa kati wa Crystal Palace Marc Guehi, 22, huku wakitafuta nafasi ya kumpa kinga William Saliba.(Express)
Juventus wanafikiria kumwajiri mkufunzi wa Marseille Igor Tudor iwapo Max Allegri ataondoka msimu huu wa joto, huku walengwa wengine Antonio Conte na Zinedine Zidane wakionekana kuwa waghali sana (Mail)
Beki wa Ajax Jurrien Timber, 21, amethibitisha kuwa anapanga kuondoka katika klabu hiyo msimu huu wa joto huku Manchester United na Liverpool zikiendelea kumtaka .(Metro)
Mshambulizi wa Crystal Palace na Ivory Coast h yuko tayari kuhamia klabu ya Ufaransa ya Marseille huku mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 30 akisemekana kuwa na hamu ya kucheza soka ya Ligi ya Mabingwa. (90 min)
Kipa anayecheza kwa mkopo wa Nottingham Forest Dean Henderson, 26, anataka kuondoka kabisa kutoka kwa klabu yake ya kudumu ya Manchester United msimu huu wa joto huku mlinda lango huyo wa Uingereza akitaka kucheza mara kwa mara.(Football Insider)
Manchester City na Brentford ziko kwenye mazungumzo na AFC Wimbledon ili kumsajili golikipa wa kimataifa wa England wa Under-16 Thorsten Brits, 15. (Fabrizio Romano)
Liverpool wameanza mazungumzo na Sporting Lisbon kuhusu uhamisho wa kiungo wa kati wa Uruguay Manuel Ugarte, 22, mwenye thamani ya pauni milioni 53, huku Leeds , Tottenham na Aston Villa pia zikiwania saini yake(O Jogo - Kwa Kireno)
Manchester United , Newcastle United na Liverpool zote zinataka kumnunua beki wa Nice Jean-Clair Todibo, 23, kwa pauni milioni 26.5 msimu huu.(L'Equipe - Kwa Kifaransa)
BBC



