Kutokana na tukio la kukatika kwa Umeme kwenye uwanja wa Benjamin Mkapa jana wakati wa mchezo wa mkondo wa pili robo fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika kati ya Yanga dhidi ya Rivers United, Serikali imechukua hatua ya kuwasimamisha kazi Wasimamizi wa uwanja ili kupisha uchunguzi wa tukio hilo ambalo limetokea kwa mara ya pili katika kipindi cha wiki sita
Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo Dk Pindi Chana ameagiza kusimamishwa kazi kwa watumishi wanaohusika na uendeshaji wa uwanja wa Mkapa ambao ni Kaimu Meneja wa Uwanja Salum Mtumbuka, Mhandisi wa Umeme Manyori Juma Kapesa na Afisa Tawala wa Uwanja Tusege Nikupala
Watumishi wengine waliosimamishwa kazi ambao wana jukumu la kusimamia uwanja ni Gordon Nsajigwa, Gabriel Mwasele, Yanuaria Imboru na Dk Christina Luambano
Aidha Katibu Mkuu wa Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo amemteua Milinde Mahona kuwa Kaimu Meneja wa uwanja
