Azam Fc yashusha kocha Msenegal

Joel JJ By Joel JJ β€’ 1st May 2023


Azam Fc yashusha kocha Msenegal

Klabu ya Azam Fc imemtambulisha kocha Mkuu Mpya raia wa Senegal Youssouph Dabo, ambaye ataanza majukumu yake kuanzia Msimu ujao wa 2023/24

Dabo, amesaini mkataba wa miaka mitatu mchana wa leo mbele ya Mtendaji Mkuu wa Azam Fc Abdulkarim Amin 'Popat'

Azam Fc imejipanga kukisuka upya kikosi, wakimpa kocha huyo muda wa kuiangalia timu na kufanya maboresho muhimu kabla kuanza majukumu yake wakati ya pre-season kuelekea msimu ujao

Azam tayari imejihakikishia tiketi ya kushiriki michuano ya kombe la Shirikisho barani Afrika msimu ujao


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.