Klabu ya Azam Fc imemtambulisha kocha Mkuu Mpya raia wa Senegal Youssouph Dabo, ambaye ataanza majukumu yake kuanzia Msimu ujao wa 2023/24
Dabo, amesaini mkataba wa miaka mitatu mchana wa leo mbele ya Mtendaji Mkuu wa Azam Fc Abdulkarim Amin 'Popat'
Azam Fc imejipanga kukisuka upya kikosi, wakimpa kocha huyo muda wa kuiangalia timu na kufanya maboresho muhimu kabla kuanza majukumu yake wakati ya pre-season kuelekea msimu ujao
Azam tayari imejihakikishia tiketi ya kushiriki michuano ya kombe la Shirikisho barani Afrika msimu ujao




