Yanga - Local

Yanga yalia ya ratiba Ligi Kuu, FA

Joel JJ By Joel JJ
β€’
2 May 2023
Yanga yalia ya ratiba Ligi Kuu, FA

Rais wa Yanga Injinia Hersi Said amesema wameiandikia barua Bodi ya Ligi Kuu kuomba 'review' ya Ratiba kutokana na mfululizo wa mechi zinazowakabili

Jana Yanga ilikwama kutua Dodoma wakati ikiwa safarini kuelekea Singida na kulazimika kurejea jijini Dar es salaam kutokana na changamoto ya taa kwenye uwanja wa Ndege wa Dodoma

Injinia Hersi amesema wanafanya utaratibu kuhakikisha timu inasafiri mkoani Singida haraka iwezekanavyo kwa ajili ya mchezo wa ligi kuu dhidi ya Singida Big Stars ambao utapigwa Alhamisi, May 04 katika uwanja wa Liti

"Tunawasiliana na Mamlaka za soka nchini, tumewaomba wafanye review ya ratiba ya mechi zetu kwani sio rafiki kwa afya za wachezaji"

"Tunapaswa kucheza na Singida BS mechi ya ligi kuu May 04 halafu kucheza nao tena mechi ya nusu fainali kombe la FA May 07"

"Tunakabiliwa na mchezo wa nusu fainali kombe la Shirikisho la CAF May 10, tunapaswa kusafiri kutoka Singida kurejea Dar baada ya mchezo dhidi ya Singida BS May 07"

"Hakuna usafiri wa ndege kutoka Singida kuja Dar maana yake ni kuwa tutalazimika kusafiri kwa njia ya basi mpaka Dodoma na tutafika Dar May 08 kwa hiyo tutakuwa na siku moja tu ya kujiandaa na mchezo wa nusu fainali ya CAF"

"Wanasema mcheza kwao hutuzwa, tukiwa wawakilishi wa nchi tumeomba tupewe muda wa kujiandaa na mchezo dhidi ya Malumo Galants," alisema Hersi

More Stories

Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
9h ago
READ MORE β†’
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
9h ago
READ MORE β†’
Highlights : Azam Fc 0-2 Simba
Highlights : Azam Fc 0-2 Simba
9h ago
READ MORE β†’
Mizizima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
Mizizima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
13h ago
READ MORE β†’
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
16h ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
17h ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
17h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
18h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
19h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
20h ago
READ MORE β†’