Sam Allardyce amekubali kurejea katika usimamizi wa Premier League kama bosi mpya wa Leeds United, talkSPORT imeripoti
Leeds wamemfuta kazi Javi Gracia mapema leo Jumanne, huku kocha wa zamani wa Uingereza Allardyce akiwa tayari kuchukua mikoba ya michezo minne ya mwisho ya Ligi Kuu ya Uingereza msimu huu
Gracia aliteuliwa mwezi Februari na Allardyce atakuwa kocha mkuu wa nne wa Leeds msimu huu baada ya Jesse Marsch na Michael Skubala
Mkurugenzi wa michezo Victor Orta, ambaye alimwajiri Gracia, pia ana uwezekano wa kuacha jukumu lake baada ya majadiliano ya kina ya baraza siku ya Jumatatu
Tony Pulis, 65, na nyota wa zamani wa United Lee Bowyer, pia wamezingatiwa kama chaguo la mlezi wa Leeds
Jukumu la mwisho la meneja wa Stoke Pulis lilikuwa kama bosi wa Sheffield Wednesday, ambayo ilidumu mwezi mmoja tu mnamo 2020
Bowyer, 46, ambaye alitumia miaka saba Elland Road kama mchezaji kati ya 1996 na 2003, mara ya mwisho aliiongoza Birmingham City ambapo alitimuliwa mwaka 2022
Lakini inaonekana kana kwamba Allardyce ndiye mtu atakayepewa jukumu la kujaribu kuibakisha Leeds kwenye ligi kuu
Mzee huyo mwenye umri wa miaka 68 amekuwa nje ya usimamizi kwa miaka miwili. Jukumu lake la mwisho lilikuwa West Brom, alipoteuliwa katikati mwa msimu lakini hakuweza kuwanusuru na kushuka daraja



