Ripoti kutoka Ufaransa zimebainisha kuwa Paris Saint-Germain (PSG) imemsimamisha kwa wiki mbili Mchezaji wake Lionel Messi kutokana na utovu wa nidhamu
Imeelezwa kuwa Messi alisafiri kwenda Saudi Arabia wiki hii bila ruhusa ya klabu
PSG imeripotiwa kumsimamisha Messi kwa wiki mbili bila malipo baada ya kutohudhuria mazoezi bila kibali na kusafiri kwenda Saudi Arabia ambako alionekana akiwa kwenye Mji wa Riyadh siku ya Jumatatu
Mkataba wa Messi na PSG unamalizika mwishoni mwa msimu, pengine ni wazi sasa Messi hataendelea kuitumikia timu hiyo