Erling Haaland alipewa heshima na wachezaji wenzake wa Manchester City baada ya kuvunja rekodi ya kufunga mabao katika msimu wa Ligi Kuu ya Uingereza.
Mshambuliaji huyo wa Manchester City alifunga bao lake la 35 la ligi dhidi ya West Ham katika ushindi wa mabao 3-0
Wachezaji wa Manchester City walitengeneza mistari miwili na Haaland kupitia katikati huku wakimpongeza kwamafanikio aliyopata
Halaand alihitaji bao moja pekee kuvunja rekodi iliyowekwa na Alan Shearer na Andy Cole, ambao wote walifunga mabao 34
Shearer alifunga mabao 34 msimu wa 1994/95 akiwa na Blackburn huku Cole akifunga mabao 34 msimu wa 1993/94 alipokuwa akiichezea Newcastle.



