Simba - Azam - Local

Tuko tayari kwa nusu fainali FA - Mgunda

Joel JJ By Joel JJ
β€’
6 May 2023
Tuko tayari kwa nusu fainali FA - Mgunda

Simba iko tayari kwa mchezo wa nusu fainali kombe la Shirikisho la Azam (ASFC) dhidi ya Azam Fc ambao utapigwa Jumapili, May 07 katika uwanja wa Nangwanda Sijaona mkoani Mtwara

Kocha Msaidizi wa Simba Juma Mgunda amesema wachezaji wote wako katika hali nzuri kuelekea mchezo huo ambao wanatarajia utakuwa mgumu

"Maandalizi ya mchezo yamekamilika, wachezajii wote wako kwenye hali nzuri. Tunajua utakuwa mchezo mgumu, tunawaheshimu Azam Fc kwa kuwa ni timu nzuri"

"Hata hivyo sisi tumejipanga tukihitaji kushinda ili tuweze kuingia fainali ya michuano hii," alisema Mgunda

Akizungumzia maandalizi ya mchezo, Mgunda amesema watakuwa na mabadiliko ya kimbinu kwa sababu utakuwa mchezo wa mtoano ambao lazima mshindi apatikane

Amesema Azam Fc walipata matokeo mazuri dhidi ya Simba kwenye ligi hivyo watahitaji kuwa bora kimbinu ili kuhakikisha wanapata ushindi

"Katika mechi za ligi msimu huu wamefanya vizuri dhidi yetu lakini mchezo wa kesho ni tofauti na mtoano kwahiyo hata mbinu zitakuwa tofauti, tumejipanga kwa ajili ya kupata ushindi"

Nae nahodha Msaidizi wa Simba Mohammed Hussein 'Zimbwe Jr' amesema matumaini ya Simba kushinda taji msimu huu yamebaki katika kombe la FA hivyo watapambana kuhakikisha wanapata ushindi

"Matumaini yetu yamebaki zaidi kwenye michuano hii, tunajua ugumu na umuhimu wa mchezo lakini tupo tayari kupambana kuhakikisha tunapata ushindi," alisema

More Stories

Mizzima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
Mizzima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
3h ago
READ MORE β†’
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
7h ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
7h ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
8h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
9h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
9h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
10h ago
READ MORE β†’
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
10h ago
READ MORE β†’
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
1d ago
READ MORE β†’
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
1d ago
READ MORE β†’