Azam - Local - Transfer

Kipa Rivers United aitamani Azam Fc

Joel JJ By Joel JJ
β€’
8 May 2023
Kipa Rivers United aitamani Azam Fc

Mlinda lango wa Rivers United ya nchini Nigeria, Victor Sochima ameweka wazi malengo yake msimu ujao ni kucheza timu kubwa hapa Tanzania huku akitaja miongoni mwao zinazomvutia ni matajiri wa jiji la Dar es Salaam, Azam FC

Sochima alionyesha kiwango kizuri katika michezo yote miwili ya hatua ya robo fainali ya Kombe la Shirikisho Afrika dhidi ya Yanga hali iliyozifanya baadhi ya timu nchini kuanza mazungumzo naye ya kimya kimya

Sochima amesema timu nyingi zimefurahishwa na uwezo wake hivyo zilimfuata kuzungumza naye ingawa kwa sasa akili yake ameiwekeza kwa ajili ya kuhakikisha msimu huu unaisha

"Siwezi kuweka wazi kwenye kila kitu kinachoendelea lakini itoshe kusema ni kweli nimefuatwa na baadhi ya timu ikiwemo Yanga kwa sababu baada ya mechi yetu kuisha nilifuatwa na kocha wao, Nasreddine Nabi," alisema

Sochima aliongeza mbali na Yanga ila timu nyingine ambayo imeonyesha nia ya kuhitaji saini yake ni Azam ambayo kwake binafsi anatamani kuichezea kwani miundombinu iliyonayo inamshawishi tofauti na kwingine

"Pale Azam kuna rafiki yangu mkubwa anaitwa, Isah (Ndala) ni mchezaji mzuri ambaye nimekuwa naye kwa ukaribu hivyo nitafurahia kama itatokea siku moja tutacheza wote pamoja ingawa kwa sasa dili bado halijakamilika," alisema

More Stories

Mizzima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
Mizzima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
2h ago
READ MORE β†’
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
6h ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
6h ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
7h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
8h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
8h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
9h ago
READ MORE β†’
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
9h ago
READ MORE β†’
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
22h ago
READ MORE β†’
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
23h ago
READ MORE β†’