Mkakati wa Yanga ni kuibuka na ushindi kwenye mchezo wa mkondo wa kwanza nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika dhidi ya Marumo Gallants ambao utapigwa Jumatano, May 10 katika uwanja wa Benjamin Mkapa
Tayari Yanga imeandika rekodi kwa kuwa timu ya kwanza Tanzania kutinga nusu fainali ya michuano ya kombe la Shirikisho barani Afrika
Kutokana na ubora wa kikosi cha Yanga msimu huu, Yanga ina nafasi kubwa ya kufanya vizuri zaidi katika michuano hiyo sasa wakiisaka fainali
Mkakati wa kutinga fainali unaanzia nyumbani Yanga ikihitaji ushindi dhidi ya Marumo Gallants ili kuhakikisha inakwenda kukata tiketi ya fainali kwenye mchezo wa marudiano wiki ijayo
Afisa Habari wa Yanga Ali Kamwe amewataka mashabiki wa Yanga kununua tiketi zao mapema ili kuwa sehemu ya historia inayokwenda kuandikwa siku ya Jumatano
OUR TEAM, OUR TIME ni kauli mbiu maalum inayotumiwa na Yanga kuelekea mchezo huo







