Baada ya kurejea jijini Dar es salaam kutoka mkoani Mtwara jana, kikosi cha Simba leo kimerejea mazoezi kwa ajili ya maandalizi ya mechi tatu za kuhitimisha msimu wa ligi kuu ya NBC
Ijumaa May 12 Simba itashuka uwanja wa Azam Complex, Chamazi kuikabili Ruvu Shooting katika mchezo wa ligi kuu ya NBC, raundi ya 28
Mchezo utakaofuata ni dhidi ya Polisi Tanzania kabla ya kuhitimisha msimu kwa mchezo dhidi ya Coastal Union May 28
Mechi zote zitapigwa uwanja wa Azam Complex, Chamazi jijini Dar es salaam



