Simba yaanza mawindo ya Ruvu Shooting

Joel JJ By Joel JJ β€’ 9th May 2023


Simba yaanza mawindo ya Ruvu Shooting

Baada ya kurejea jijini Dar es salaam kutoka mkoani Mtwara jana, kikosi cha Simba leo kimerejea mazoezi kwa ajili ya maandalizi ya mechi tatu za kuhitimisha msimu wa ligi kuu ya NBC

Ijumaa May 12 Simba itashuka uwanja wa Azam Complex, Chamazi kuikabili Ruvu Shooting katika mchezo wa ligi kuu ya NBC, raundi ya 28

Mchezo utakaofuata ni dhidi ya Polisi Tanzania kabla ya kuhitimisha msimu kwa mchezo dhidi ya Coastal Union May 28

Mechi zote zitapigwa uwanja wa Azam Complex, Chamazi jijini Dar es salaam


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.