Klabu ya Marumo Gallants kutoka Afrika Kusini imetua nchini Alfajiri ya leo Jumanne kuelekea mchezo wa mkondo wa kwanza nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika dhidi ya Yanga
Mtanange huo utapigwa kesho Jumatano, May 10 katika uwanja wa Benjamin Mkapa, saa 10 jioni
Baada ya kuwasili Marumo hawakutaka kuzungumza na mtu yeyote ikiwa ni pamoja na wanahabari huku timu hiyo ikigoma kupanda basi waliloandaliwa na Yanga
Waliondoka uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere kwa kutumia usafiri wa basi dogo
Marumo wamekuwa na matokeo ya kushangaza katika mashindano ya CAF ya Shirikisho wakifanikiwa kutinga nusu fainali huku kwenye ligi ya Afrika Kusini wakipambana kujinusuru kushuka daraja
Marumo wanashinda nafasi ya 14 katika timu 16 wakiwa alama tatu juu ya eneo la hatari kushuka daraja



