Manchester United wamefanya mazungumzo na Benfica kuhusu mkataba wenye thamani ya hadi £100m, ikijumuisha nyongeza, kwa ajili ya mshambuliaji wa Ureno Goncalo Ramos, 21. (Mirror)
Chelsea wanatumai kuwa uteuzi wa Mauricio Pochettino kama meneja unaweza kumshawishi kiungo wa Ufaransa N'Golo Kante, 32, kusaini mkataba mpya Stamford Bridge. (Telegraph - usajili unahitajika)
Chelsea wako tayari kumtoa mshambuliaji wa Gabon Pierre-Emerick Aubameyang, 33, na mlinzi wa Uhispania Marc Cucurella, 24, katika mpango wa kubadilisha mkopo wa mshambuliaji wa Ureno Joao Felix, 23, kutoka Atletico Madrid kuwa mkataba wa kudumu. (Standard)
Manchester United wako tayari kumenyana na Arsenal na Chelsea i, kwa ajili ya kuinasa saini ya Declan Rice baada ya kufurahishwa na kiwango cha kiungo huyo wa Uingereza mwenye umri wa miaka 24 akiwa na West Ham dhidi ya Mashetani Wekundu siku ya Jumapili. (Sun)
West Ham wanavutiwa na mshambuliaji wa Coventry City mwenye umri wa miaka 24 Viktor Gyokeres. (Mirror)
Arsenal wana matumaini kuwa winga wa Uingereza Bukayo Saka, 21, atasaini mkataba mpya wa miaka mitano wenye thamani ya pauni 300,000 kwa wiki kabla ya mwisho wa msimu huu. (TalkSPORT)
Newcastle ni miongoni mwa vilabu kadhaa vya Ligi ya Premia vinavyotarajiwa kumenyana na Inter Milan na Juventus kuwania saini ya beki wa Monza Mbrazil Carlos Augusto, 24. (Clciomercato)
Liverpool wapo kwenye mazungumzo ya juu ya kumteua Mjerumani Jorg Schmadtke kuwa mkurugenzi wao mpya wa michezo. (Mail)
Meneja wa Fulham Marco Silva ana kipengele cha kuachiliwa kwa pauni milioni 6 katika kandarasi yake na West Ham akizingatia mbinu ya kumnunua Mreno huyo mwenye umri wa miaka 45 iwapo wataamua kumfuta kazi David Moyes mwishoni mwa msimu huu. (Mail)
David de Gea amekubali kusaini mkataba mpya na Manchester United kwa masharti yaliyopunguzwa lakini hakuna uhakika kwamba mlinda mlango huyo wa Uhispania mwenye umri wa miaka 32 atakuwa nambari moja wa klabu hiyo. (Telegraph - usajili unahitajika)
Kiungo wa kati wa zamani wa Uingereza James Milner, 37, alikataa ofa kutoka kwa Everton ili ajiunge na Brighton mara tu kandarasi yake ya Liverpool itakapokamilika msimu huu wa joto. (Football Insider)
Kocha wa zamani wa West Brom na Barnsley Valerien Ismael amepiga hatu katika mazungumzo ya kuwa meneja wa Watford. (Athletic- Usajili unahitajika)
BBC



