JKT - Local

Hitimana kuibukia JKT Tanzania

Joel JJ By Joel JJ
β€’
11 May 2023
Hitimana kuibukia JKT Tanzania

Baada ya kufanikiwa kurejesha timu Ligi Kuu Tanzania Bara kuelekea msimu mpya wa 2023/24, uongozi wa Klabu ya JKT Tanzania upo katika mchakato wa kumpa ajira, aliyekuwa Kocha Mkuu wa KMC FC, Thierry Hitimana, kukinoa kikosi hicho kwa msimu ujao, imefahamika

Licha ya uongozi wa JKT Tanzania kutoweka wazi suala hilo huku wakidai kuwa wataendelea na Kocha Hamsini Malale aliyeipandisha timu hiyo Ligi Kuu endapo anahitaji kuendelea kubaki katika timu hiyo, lakini taarifa za ndani zimedokeza kuwa klabu hiyo ipo katika mazungumzo na Hitimana.

Hata hivyo, Malale alipoulizwa juu ya mustakbali wake juu ya maboresho ya kikosi chake, alisema hawezi kuweka mipango yake ya usajili ya msimu ujao kwa sababu hajui hatima yake.

Alipotafutwa Hitimana mwenyewe akagoma kuweka wazi dili hilo akisisitiza kuwa hakuna timu iliyomfuata

"Hakuna kiongozi aliyenifuata kwa ajili ya mazungumzo yoyote, hilo suala kama lipo, kwangu ni vizuri kwa sababu hakuna mtu anayekataa kazi anapoipata," alisema Hitimana

Hitimana ni kocha mwenye uzoefu wa Ligi kuu ya Tanzania Bara akiwa amewahi kuzifundisha Namungo Fc na Simba kabla ya kujiunga na KMC

More Stories

Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
5h ago
READ MORE β†’
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
5h ago
READ MORE β†’
Highlights : Azam Fc 0-2 Simba
Highlights : Azam Fc 0-2 Simba
5h ago
READ MORE β†’
Mizizima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
Mizizima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
9h ago
READ MORE β†’
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
12h ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
13h ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
13h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
14h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
15h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
16h ago
READ MORE β†’