Simba - Local

Bodi Simba yaomba radhi Wanachama

Joel JJ By Joel JJ
β€’
12 May 2023
Bodi Simba yaomba radhi Wanachama

Bodi ya Wakurugenzi klabu ya Simba imewaomba radhi Wanachama na mashabiki wa timu hiyo baada ya kushindwa kufikia malengo msimu huu

Mwenyekiti wa Bodi Salim Abdallah 'Try Again' amesema hakuna anayepaswa kulaumiwa kutokana na kilichotokea msimu huu kwa kuwa kila mmoja alitimiza wajibu lakini ni bahati mbaya tu hawakupata matokeo waliyotarajia

"Tunawaomba radhi wanachama na mashabiki wetu baada ya kushindwa kufikia malengo yetu msimu huu, tutajipanga upya ili kuhakikisha msimu ujao tunafanya vizuri"

"Sidhani kama kuna yeyote anapaswa kulaumiwa kwa sababu sisi kama viongozi tulitimiza wajibu wetu, ni bahati mbaya tu matokeo tuliyoyatarajia hayakuwa"

"Tumefanya usajili mzuri kwa ushirikiano lakini baadhi ya wachezaji hawakufikia matarajio yetu, na hili ni kawaida hutokea. Sisi tuliwahi kumuuza Clatous Chama na Luis Miquissone wakiwa katika viwango vya juu kabisa lakini hawakufanya kile kilichotarajiwa katika timu zao mpya"

"Zipo sababu ambazo zinaweza kupelekea mchezaji asifanye vizuri, mfano kuzoea mazingira, hali ya hewa au majeruhi. Ismail Sawadogo alionyesha kiwango bora sana kwenye mchezo wake wa kwanza tulipomsajili lakini baadae akapata majeraha mwenyewe akalazimisha kutaka kuonyesha kile alichonacho matokeo yake haikuwa hivyo"

"Suala la majeruhi kwa baadhi ya wachezaji imekuwa changamoto pia, hila nadhani benchi la ufundi na madaktari wataweza kutueleza kitaam zaidi na nini kifanyike," alisema  Try Again

Try Again amesema Simba ilishinda mataji karibu yote kwa misimu minne mfululizo, wapinzani wao nao walikuwa wakijipanga katika kipindi hicho na sasa wameimarika

Hivyo ni wakati wa Simba nayo kujipanga ili kuhakikisha msimu ujao inarejesha ubabe wake katika soka la Tanzania

More Stories

Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
29m ago
READ MORE β†’
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
42m ago
READ MORE β†’
Highlights : Azam Fc 0-2 Simba
Highlights : Azam Fc 0-2 Simba
1h ago
READ MORE β†’
Mizizima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
Mizizima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
4h ago
READ MORE β†’
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
8h ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
8h ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
9h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
10h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
10h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
11h ago
READ MORE β†’