Yanga - Dodoma - Local

Yanga kutangaza ubingwa mbele ya Dodoma Jiji leo?

Joel JJ By Joel JJ
β€’
13 May 2023
Yanga kutangaza ubingwa mbele ya Dodoma Jiji leo?

Vinara wa Ligi Kuu ya NBC, Yanga jioni ya leo watashuka uwanja wa Azam Complex, Chamazi kupepetana na Dodoma Jiji katika mchezo ambao Wananchi wana nafasi ya kutwaa ubingwa kama wataibuka na ushindi

Wakiwa kileleni mwa msimamo wa ligi wakiwa na alama 71, alama nne zaidi ya Simba inayoshika nafasi ya pili, Yanga inahitaji alama tatu tu kutwaa ubingwa

Simba imesalia na mechi mbili ambazo wakishinda zote watafikisha alama 73, ushindi kwa Yanga leo utawafanya wafikishe alama 74

Ni wazi hautakuwa mchezo mwepesi kwani hata Dodoma Jiji wanahitaji matokeo mazuri ili kujihakikishia usalama wa kubaki ligi kuu msimu huu

Lakini ubora wa kikosi cha kocha Nasreddine Nabi unawapa nafasi zaidi Yanga kushinda mchezo huo na kujihakikishia ubingwa kabla ya kusafiri Afrika Kusini wanakokabiliwa na mchezo wa mkondo wa pili nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika dhidi ya Marumo Gallants. Yanga itaondoka nchini Alfajiri ya kesho Jumapili kuelekea Afrika Kusini

Afisa Habari wa Yanga Ali Kamwe amesema shamrashamra kuelekea mchezo huo zitaanza saa sita mchana ambapo kutakuwa na burudani za utangulizi kuelekea muda wa mchezo ambao ni saa 10 jioni

More Stories

Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
5h ago
READ MORE β†’
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
5h ago
READ MORE β†’
Highlights : Azam Fc 0-2 Simba
Highlights : Azam Fc 0-2 Simba
5h ago
READ MORE β†’
Mizizima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
Mizizima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
9h ago
READ MORE β†’
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
12h ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
13h ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
13h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
14h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
15h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
16h ago
READ MORE β†’