Kitoyosce yaungana na JKT Tanzania Ligi Kuu

Joel JJ By Joel JJ β€’ 14th May 2023


Kitoyosce yaungana na JKT Tanzania Ligi Kuu

Timu ya Kitayosce FC imefanikiwa kupanda Ligi Kuu ya Tanzania Bara baada ya ushindi wa mabao 3-0 dhidi ya African Sports ya Tanga jana Uwanja wa Ali Hassan Mwinyi Tabora.

Kitayosce imefikisha pointi 60, moja zaidi ya Pamba FC ambayo pia imeshinda 2-1 dhidi ya Fountain Gate Uwanja wa Nyamagana Jijini Mwanza.

Kitayosce imeungana na JKT Tanzania, mabingwa wa Championship waliomaliza na pointi 63.

Pamba itakwenda kumenyana na Mashujaa iliyomaliza na pointi 49 nafasi ya nne na mshindi wa jumla atakwenda kumenyana na timu iliyoporomoka kutoka Ligi Kuu kuwania kupanda.


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.