Polisi Tanzania imeendelea kupambana kujinusuru na kushuka daraja baada ya kupata ushindi wa mabao 3-1 dhidi ya Mtibwa Sugar katika mchezo uliopigwa uwanja wa Ushirika
Polisi Tanzania imefikisha alama 25 lakini bado inahitaji alama nne zaidi ili kuweza kuondoka kwenye eneo la kushuka daraja
Ni lazima ishinde mechi mbili zilizosalia dhidi ya Simba na Azam Fc na wakati huo huo ikiziombea Mtibwa Sugar, KMC na Dodoma Jiji zisishinde mechi zao
Ni wazi bado maafande wa Polisi Tanzania wanahitaji muujiza ili kuendelea kubaki ligi kuu




