Nyota wa Manchester City Bernardo Silva anasakwa zaidi na Paris St-Germain wanaotaka kumleta kiungo huyo wa kati wa Ureno mwenye umri wa miaka 28 kuchukua nafasi ya mshambuliaji wa Argentina Lionel Messi, 35. (Le Parisien)
Arsenal wako tayari kuipa West Ham kiasi cha £90m ambayo ni rekodi ya klabu kwa ajili ya kiungo wa kati wa England Declan Rice, 24, wakati Granit Xhaka wa Switzerland, 30, anaweza kuwa mmoja wa wachezaji watakaouzwa na The Gunners. (Mail)
Kiungo wa kati wa Argentina Alexis Mac Allister, ambaye amekuwa akihusishwa na Liverpool na Manchester United, anataka kujiunga na klabu inayocheza Ligi ya Mabingwa Ulaya ikiwa mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 24 ataondoka Brighton msimu huu wa joto. (Athletic)
Meneja mpya mtarajiwa wa Chelsea Mauricio Pochettino anatazamiwa kufanya mazungumzo na Mason Mount ili kumshawishi kiungo huyo wa kati wa England mwenye umri wa miaka 24 kuongeza mkataba wake ambao unamalizika msimu wa joto wa 2024. (Football Insider)
Bayern Munich na Borussia Dortmund zote zinamtaka kiungo wa kati wa Mexico Edson Alvarez, 25, ambaye Ajax inaweza kuwa tayari kumuuza kwa £30m. (SPORT1)
Mabeki wa Uingereza Phil Jones, 31, na Axel Tuanzebe, 25, wanatarajiwa kuuzwa na Manchester United msimu huu wa joto. (ManchesterEveningNews)
Newcastle pia wanavutiwa na kiungo wa kati wa Chelsea mwenye umri wa miaka 23 Conor Gallagher, wakati The Magpies watakabiliana na ushindani kutoka kwa Tottenham wanaomtaka mchezaji mwenzake wa kimataifa wa England anayekipiga Leicester City James Maddison. (Mail)
Manchester United wanafikiria kumnunua mlinda mlango wa Borussia Dortmund Gregor Kobel, ingawa klabu hiyo ya Ujerumani inakusudia kumpa mkataba mpya mchezaji huyo wa kimataifa wa Uswizi mwenye umri wa miaka 25. (Independent)
Tottenham wamefanya mazungumzo na mkurugenzi wa michezo wa Roma kuhusu jukumu lao la mkurugenzi wa soka. (The i Newspaper)
BBC



