Droo Super League kufanyika Tanzania

Joel JJ By Joel JJ β€’ 16th May 2023


Droo Super League kufanyika Tanzania

Kulingana na Mwandishi wa habari kutoka Misri Mohammed Saied, michuano ya CAF Africa Super league itafanyika mwezi Oktoba 2023 ambapo droo ya mechi za awali itapangwa Julai 2023 nchini Tanzania

Kwa mujibu wa Saied, timu zitawekwa kwenye makundi mawili ambapo timu ya kundi moja itapangwa na timu ya kundi la pili ambapo zitacheza mechi mbili

Timu 8 zitakazoshiriki Super League hazitaanzia mechi za awali za michuano ya CAF (Champions League, Confederation Cup) msimu ujao bali wataanzia mzunguko wa pili

Michuano inatarajiwa kuanza katikati ya mwezi Oktoba mpaka mwishoni mwa Novemba 2023


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.