Inter wameifunga AC Milan 1-0 katika mchezo wa mkondo wa pili wa nusu fainali huko San Siro Jumanne usiku, na kutinga fainali ya Ligi ya Mabingwa kwa jumla ya mabao 3-0
Lautaro Martinez alifunga bao pekee la ushindi dakika ya 74, huku Romelu Lukaku aliyetokea benchi kipindi cha pili akitengeneza pasi ya bao
Inter wanasubiri mshindi wa mechi ya marudiano ya leo kati ya Manchester City dhidi ya Real Madrid ambayo itapigwa uwanja wa Etihad
Mkufunzi wa Ac Milan Stefano Pioli alizungumza na Sky Italia baada ya kushindwa: "Wachezaji walijitolea katika mechi zote mbili. Inter walistahili kushinda na tunawapongeza. Tulikuwa na matumaini ya kufika fainali. Ni wazi nimevunjika moyo kwa kutofika fainali. Tumejifunza mengi msimu huu"