Yanga kamili kuikabili Marumo Gallants Afrika Kusini

Joel JJ By Joel JJ β€’ 17th May 2023


Yanga kamili kuikabili Marumo Gallants Afrika Kusini

Mabingwa wa soka Tanzania Bara Yanga leo wanawania rekodi ya kutinga fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika watakapowakabili Marumo Gallants katika mchezo wa mkondo wa pili wa nusu fainali utakaopigwa uwanja wa Royal Bafokeng huko Afrika Kusini

Yanga itaingia katika mchezo huo ikiwa na faida ya ushindi wa mabao 2-0 waliopata katika mchezo wa mkondo wa kwanza uliopigwa uwanja wa Benjamin Mkapa wiki iliyopita

Ni mechi ngumu ya ugenini, Marumo Gallants wakitarajiwa kujaribu kupindua matokeo katika mchezo ambao mashabiki wataingia bure

Marumo wamekuwa na matokeo ya kushangaza kwenye mashindano ya Shirikisho wakishinda mechi zote walizocheza katika uwanja wao wa nyumbani lakini timu hiyo ikipambana kujinusuru kuteremka daraja katika ligi kuu ya Afrika Kusini

Kocha Mkuu wa Yanga Nasreddine Nabi amesema watakuwa na dakika 90 za jasho na damu kuipambania Yanga na kupeperusha vyema bendera ya Tanzania huko ugenini


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.