Mabingwa wa soka Tanzania Bara Yanga leo wanawania rekodi ya kutinga fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika watakapowakabili Marumo Gallants katika mchezo wa mkondo wa pili wa nusu fainali utakaopigwa uwanja wa Royal Bafokeng huko Afrika Kusini
Yanga itaingia katika mchezo huo ikiwa na faida ya ushindi wa mabao 2-0 waliopata katika mchezo wa mkondo wa kwanza uliopigwa uwanja wa Benjamin Mkapa wiki iliyopita
Ni mechi ngumu ya ugenini, Marumo Gallants wakitarajiwa kujaribu kupindua matokeo katika mchezo ambao mashabiki wataingia bure
Marumo wamekuwa na matokeo ya kushangaza kwenye mashindano ya Shirikisho wakishinda mechi zote walizocheza katika uwanja wao wa nyumbani lakini timu hiyo ikipambana kujinusuru kuteremka daraja katika ligi kuu ya Afrika Kusini
Kocha Mkuu wa Yanga Nasreddine Nabi amesema watakuwa na dakika 90 za jasho na damu kuipambania Yanga na kupeperusha vyema bendera ya Tanzania huko ugenini



