Yanga - Singida - Local

Ni Singida BS vs Yanga nusu fainali FA leo

Joel JJ By Joel JJ
β€’
21 May 2023
Ni Singida BS vs Yanga nusu fainali FA leo

Baada ya ushindi dhidi ya Marumo Gallants ya Afrika Kusini uliowahakikishia kutinga fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika, leo Yanga inawania fainali nyingine katika mchezo wa nusu fainali kombe la Shirikisho la Azam (ASFC) dhidi ya Singida BS ambao utapigwa saa 9:30 alasiri

Kikosi cha Yanga kiliwasili mkoani Singida mapema jana na jioni kufanya mazoezi ya mwisho katia uwanja wa LITI

Huu ni mchezo wa pili kuzikutanisha Yanga na Singida BS katika uwanja wa Liti msimu huu

May 05 timu hizo zilichuana katika mchezo wa ligi kuu na Yanga kuibuka na ushindi wa mabao 2-0

Kocha Mkuu wa Singida BS Hans van Pluijm amesema wamefanya maandalizi mazuri na leo hawatarudia makosa waliyofanya katika mchezo wa uliopita kwenye ligi

Hata hivyo watalazimika kuwa katika ubora hasa kuweza kupata ushindi mbele ya Yanga ambayo wachezaji wake wana morali kubwa

Jambo pekee ambalo linaweza kuiathiri Yanga ni uchovu ambapo mabingwa hao wa Tanzania Bara wamefanya mazoezi mara moja tu tangu watoke Afrika KusiniΒ 

Baada ya ushindi dhidi ya Marumo May 17, Yanga iliondoka Afrika Kusini jioni ya May 18 na kuwasili jijini Dar es salaam Alfajiri ya May 19 ambapo siku hiyo jioni wakaunganisha kuelekea mkoani Dodoma ambako timu ililala

Jana May 20 asubuhi Wananchi wakaelekea mkoani Singida na jioni wakafanya mazoezi yao ya kwanza tangu walipochuana na Marumo

Hata hivyo Kocha Msaidizi wa Yanga Cedric Kaze alisema watakuwa na mabadiliko ya kikosi katika mchezo huo na wanafurahi kuwa na kikosi kipana wachezaji wote wako tayari

Mtanange huo utakuwa na dakika 30 za nyongeza kama hakutapatikana mshindi kwenye dakika 90 na baadae kupigwa mikwaju ya penati kama mchezo utamalizika kwa sare

More Stories

Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
31m ago
READ MORE β†’
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
43m ago
READ MORE β†’
Highlights : Azam Fc 0-2 Simba
Highlights : Azam Fc 0-2 Simba
1h ago
READ MORE β†’
Mizizima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
Mizizima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
4h ago
READ MORE β†’
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
8h ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
8h ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
9h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
10h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
10h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
11h ago
READ MORE β†’