Simba - Local

Robertinho kusimamia usajili Simba

Joel JJ By Joel JJ
β€’
23 May 2023
Robertinho kusimamia usajili Simba

Kocha wa Simba, Robert Oliveira 'Robertinho', amesem anataka ashirikishwe katika kila hatua ya usajili watakaofanya kuelekea msimu ujao baada ya kukabidhi faili la majina ya wachezaji anaowataka kwenye kikosi chake

Kocha huyo raia wa Brazil amesema ili kupata wachezaji ambao wanakidhi mahitaji yake, anataka ashirikishwe kwenye kila hatua ya usajili

Msimu huu haukuwa mzuri kwa Simba baada ya kushindwa kufikia malengo waliyojiwekea mwanzoni mwa msimu

Simba walikuwa na malengo ya angalau kucheza hatua ya nusu fainali ya Ligi ya Mabingwa Afrika pamoja na kuchukua ubingwa wa Ligi Kuu Tanzania Bara na kombe la Shirikisho (FA), hata hivyo wameshindwa kufikia malengo hayo na kushuhudia watani zao, Yanga wakichukua ubingwa wa Ligi Kuu na kutinga hatua ya fainali katika michuano ya Shirikisho Afrika na ile ya FA.

"Nashukuru Mungu kwa sasa tunasubiria kumaliza msimu kwa mechi mbili zilizobakia kabla ya kuanza maandalizi ya msimu ujao, ingawa tumeanza mikakati mapema ya kujua mahitaji gani ambayo tunaweza kuyahitaji kuelekea msimu ujao kwa sababu msimu huu hakuna ambacho tumeweza kukipata"

"Kuhusu suala la usajili tayari tumeanza mikakati kwa sababu tunaelewa tumekosea wapi na kitu gani tunapaswa kufanya ili tuweze kuwa bora msimu ujao hivyo ni jambo jema kuweza kutambua kila hatua ya usajili wa wachezaji ambao tumelenga kuwasajili kupitia viongozi na ripoti itakavyoweza kuonyesha mahitaji yetu ya msimu ujao, " alisema Robertinho

Alisema kwa sasa wanaangalia michezo miwili iliyobakia na amewataka wachezaji wake kupambana kushinda mechi mbili zilizosalia ili kumaliza ligi hiyo kwa heshima.

Wachezaji wa Simba walipewa mapumziko baada ya mechi za kuhitimisha msimu kusogezwa mbele hadi Juni 06 na Juni 09 wakitarajiwa kurejea mazoezini May 24

More Stories

APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
1h ago
READ MORE β†’
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
5h ago
READ MORE β†’
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
7h ago
READ MORE β†’
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
9h ago
READ MORE β†’
Rasmi: JoΓ£o Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
Rasmi: JoΓ£o Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
11h ago
READ MORE β†’
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
11h ago
READ MORE β†’
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
11h ago
READ MORE β†’
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
13h ago
READ MORE β†’
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
17h ago
READ MORE β†’
UEFA champions league: matokeo ya usiku
UEFA champions league: matokeo ya usiku
1d ago
READ MORE β†’