Kocha wa PSG, Christophe Galtier amethibitisha kuwa nyota wake Lionel Messi ataondoka klabuni hapo mwisho wa msimu huu.
Akizungumzia hilo kocha huyo amesema anajivunia kumfundisha mchezaji huyo bora katika historia ya soka duniani.
"Jumamosi itakuwa mechi yake ya mwisho kwa Messi tutakapocheza dhidi ya Clermont," amesema Galtier
Messi anahusishwa asilimia kubwa kurudi klabu yake aliyotoka Barcelona baada ya kocha Xavi kuonyesha nia ya kumuhitaji msimu ujao
Lakini pia ana ofa nono kutoka Saudi Arabia



