Fainali ya Kombe la FA 2023 kati ya Manchester City na Manchester United itachezwa katika uwanja wa Wembley leo Jumamosi saa kumi na moja jioni kwa saa za Afrika Mashariki
Ni fainali ya kwanza inayojumuisha timu mbili za Manchester katika historia ya mashindano hayo
Mashabiki karibu 90,000 wanatarajiwa katika uwanja wa Wembley licha ya mgomo wa kitaifa wa treni uliowaathiri maelfu ya mashabiki ambao wamelazimika kuweke mipango mbadala ya usafiri hadi London
Man City inayonolewa na Pep Guardiola, tayari limeshinda Ligi ya Premia na itakutana na Inter Milan katika fainali ya Ligi ya Mabingwa mnamo Juni 10, linahitaji ushindi ili kusalia kwenye mpango wa kutwaa mataji matatu
Lakini Man United, ambao tayari wameishinda City msimu huu, wanawania taji la pili msimu huu kufuatilia ushindi wao wa Kombe la Carabao mwezi Februari