Transfer - International

Tetesi za usajili Alhamisi, Juni 08 2023

Joel JJ By Joel JJ
8 Jun 2023
Tetesi za usajili Alhamisi, Juni 08 2023

Beki wa Korea Kusini Kim Min-jae, 26, anakaribia kujiunga na Manchester United kwa mkataba wa miaka mitano kutoka Napoli. (Nicolo Schira)

Lakini Newcastle wanaweza kuteka nyara mpango huo baada ya kufanya mazungumzo na Kim, ambaye ana kipengele cha kutoa pauni milioni 42 ambacho kitaanza kutumika tarehe 1 Julai. (Sun)

Aston Villa wana nia ya kumsajili beki wa Manchester United na England Harry Maguire, 30, msimu huu wa joto. (Football Insider)

Villa pia wametoa ofa rasmi ya kumsajili beki wa Villarreal na Uhispania Pau Torres, 26. (Mirror)

Bayern Munich bado wana matumaini ya kumshawishi mshambuliaji wa Tottenham na Uingereza Harry Kane, 29, kujiunga nao licha ya kumtaka Real Madrid. (Athletic-Usajili unahitajika)

Manchester City wako tayari kumtafuta mlinzi wa RB Leipzig wa Croatia Josko Gvardiol, 21. (90min).

Al-Hilal ilifanya jaribio la mwisho kumsajili mshambuliaji wa Argentina Lionel Messi kwa kumpa mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 35 euro 500m kwa msimu. (Helena Condis Edo)

Kipa wa Inter Miami Mholanzi Nick Marsman, 32, anasema klabu hiyo ya Marekani "haiko tayari" kumkaribisha Messi. (ESPN, via Express US)

Kiungo wa kati wa Chelsea na Ufaransa N'Golo Kante, 32, amekamilisha vipimo vya afya baada ya kukubali kujiunga na Al-Ittihad kwa mkataba wa miaka miwili wenye thamani ya euro 100m (£86m) kwa msimu. (Guardian)

Kipa wa Uhispania na Manchester United David de Gea, 32, hana nia ya kujiunga na klabu ya Saudi Arabia. (Talksport)

AC Milan bado wana hamu ya kumsajili kiungo wa Uingereza Ruben Loftus-Cheek, 27, huku mazungumzo yakiendelea kuhusu uwezekano wa kuhama kutoka Chelsea. (Football Insider)

Mshambulizi wa Arsenal Folarin Balogun ananyatiwa na AC Milan na Inter Milan, huku Mmarekani huyo mwenye umri wa miaka 21 akitarajiwa kuondoka msimu huu wa joto baada ya kucheza kwa mkopo Reims. (Mail)

Brighton wanatayarisha dau la pauni milioni 40 kumsajili beki wa Uingereza Levi Colwill baada ya mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 20 kushawishika kwa mkopo kutoka Chelsea msimu uliopita. (90 min)

Manchester United wanakaribia kufanya uhamisho wa kushtukiza kwa mlinzi wa Monaco na Ufaransa Axel Disasi, 25. (L'Equipe - kwa Kifaransa)

Luton Town wamejiunga na mbio za kumsajili mlinzi mahiri wa Jamaica Joel Latibeauudiere, 23, kwa uhamisho huru kutoka Swansea City. (Football Insider)

BBC

More Stories

BREAKING: Tajiri wa Chelsea Boehly ang’atuka kwenye klabu
BREAKING: Tajiri wa Chelsea Boehly ang’atuka kwenye klabu
53m ago
READ MORE →
Ngorongoro Heroes yaweka malengo makubwa CECAFA U20
Ngorongoro Heroes yaweka malengo makubwa CECAFA U20
1h ago
READ MORE →
Yanga SC kukipiga mchezo wa kirafiki na St George uwanja wa Uhuru
Yanga SC kukipiga mchezo wa kirafiki na St George uwanja wa Uhuru
2h ago
READ MORE →
Messi aongeza taji jingine, afikisha mataji 49 katika kazi yake
Messi aongeza taji jingine, afikisha mataji 49 katika kazi yake
2h ago
READ MORE →
Raphinha, Yamal wampa wakati mgumu Mbappe mbio za ufungaji bora La liga
Raphinha, Yamal wampa wakati mgumu Mbappe mbio za ufungaji bora La liga
2h ago
READ MORE →
Manchester United yaanguka Old Trafford, yatupwa nje kwenye Carabao
Manchester United yaanguka Old Trafford, yatupwa nje kwenye Carabao
2h ago
READ MORE →
SimbaSC yatuma ujumbe mzito kwa  Yanga SC “Your next: Yanga”
SimbaSC yatuma ujumbe mzito kwa Yanga SC “Your next: Yanga”
3h ago
READ MORE →
Barcelona yaendeleza dozi La Liga, yaipiga Racing Santander 7-2
Barcelona yaendeleza dozi La Liga, yaipiga Racing Santander 7-2
4h ago
READ MORE →
Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
15h ago
READ MORE →
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
15h ago
READ MORE →