Ligi Kuu NBC inafika tamati leo

Joel JJ By Joel JJ β€’ 9th June 2023


Ligi Kuu NBC inafika tamati leo

Ligi Kuu ya NBC 2022/23 inafika tamati leo kwa timu zote 16 kushuka viwanjani majira ya saa 9:30 Alasiri

Tayari timu nne za juu ya msimamo na timu mbili za chini ya msimamo zimefahamika

Yanga, Simba, Azam Fc na Singida BS zimejihakikishia kumaliza nafasi nne za juu ambapo Yanga watakabidhiwa ubingwa baada ya mchezo dhidi ya Tanzania Prisons

Polisi Tanzania na Ruvu Shooting zimemaliza nafasi mbili za chini na hivyo zimeshuka daraja moja kwa moja

Hatma ya timu mbili zinazokwenda kucheza play-off itafahamika baada ya mechi za leo

Mbeya City na KMC zitachuana katika mchezo ambao utaamua kama zote zitacheza play-off au mshindi atanusurika?

Mtibwa Sugar nayo itahitaji kushinda dhidi ya Geita Gold ili kujihakikishia usalama wakati Coastal Union ambayo iko ugenini uwanja wa Uhuru dhidi ya Simba nayo iahitaji ushindi au alama moja ili kuwa salama


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.