Yanga - Simba - Local

Simba, Yanga zatawala tuzo TFF

Joel JJ By Joel JJ
β€’
13 Jun 2023
Simba, Yanga zatawala tuzo TFF

Kiungo mshambuliaji wa Simba Saido Ntibazonkiza usiku wa kuamkia leo aliibuka na tuzo tatu katika hafla ya utolewaji tuzo ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) kwa msimu wa 2022/23

Saido alishinda tuzo ya mfungaji bora wa Ligi Kuu, kiungo bora wa Ligi Kuu na tuzo ya FAIR PLAY

Mshambuliaji wa Yanga Fiston Mayele ndiye mchezaji bora wa msimu akiondoka na tuzo tatu, mfungaji bora na tuzo kubwa ya MVP pamoja na tuzo ya goli bora la msimu

Mayele yuko Cameroon katika majukumu ya timu ya Taifa, tuzo zake zilipokewa na mkewe kwa niaba yake

Kocha wa Yanga Nasreddine Nabi akaondoka na tuzo ya kocha bora wa msimu wakati Dickson Job akiondoka na tuzo ya beki bora wa msimu

Clement Mzize nae akabeba tuzo ya mchezaji bora chipukizi wakati Djigui Diarra akiondoka na tuzo ya kipa bora kombe la FA na Ligi Kuu

Nahodha wa Yanga Bakari Nondo Mwamnyeto akabeba tuzo ya mchezaji bora wa michuano ya kombe la Shirikisho la Azam (ASFC)

Simba imetoa wachezaji sita katika kikosi cha msimu huku Yanga ikitoa wachezaji wanne na mmoja kutoka Singida BS

Shomari Kapombe, Mohammed Hussein, Hennock Inonga, Mzamiru Yassin, Clatous Chama na Saido Ntibazonkiza wa Simba wamejumuishwa katika kikosi hicho wakati Djigui Diarra, Dickson Job, Bakari Nondo Mwamnyeto na Fiston Mayele ni upande wa Yanga wakati Bruno Gomez akitokea Singida BS

More Stories

Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
4h ago
READ MORE β†’
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
4h ago
READ MORE β†’
Highlights : Azam Fc 0-2 Simba
Highlights : Azam Fc 0-2 Simba
5h ago
READ MORE β†’
Mizizima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
Mizizima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
8h ago
READ MORE β†’
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
12h ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
12h ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
13h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
14h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
14h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
15h ago
READ MORE β†’