Arsenal wanakaribia kufikia makubaliano ya pauni milioni 100 kumsaini kiungo wa kati wa West Ham na Muingereza Declan Rice, 24. (Guardian) Meneja wa Manchester City Pep Guardiola anapanga kuondoka katika klabu hiyo mkataba wake utakapokamilika mwaka wa 2025. (Guardian)
RB Leipzig itahitaji ada ya angalau £75m ikiwa wanataka kumuuza mlinzi wa Croatia Josko Gvardiol, 21, kwa Manchester City. (Sport)
Manchester City ilikataa ofa ya Paris St-Germain ya kuwajumuisha kiungo wa kati wa Italia Marco Verratti, 30, na kipa wa Italia Gianluigi Donnarumma, 24, kama sehemu ya makubaliano ya kumsajili mchezaji wa Ureno Bernardo Silva kutoka kwa washindi wa Treble. (Footmercato – In French)
Arsenal wanahofia Chelsea wanaweza kuwashinda katika kumsajili kiungo wa kati wa Brighton Moises Caicedo, 24, kwa kumpa mchezaji huyo wa kimataifa wa Ecuador pesa zaidi. (football Transfers)
Chelsea wamemfanya mchezaji wa kimataifa wa Cameroon Andre Onana kuwa mchezaji wanayemlenga sana sana huku wakitafuta mlinda mlango mpya na Inter Milan wanataka angalau £50m kwa mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 27. (Evening Standard)
Manchester United wanaendelea na mazungumzo na Chelsea kuhusu kiungo wa kati wa Uingereza Mason Mount lakini bado kuna pengo la tathmini kati ya vilabu hivyo viwili kwa mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 24. (Sky Sports)
Manchester United hawana uwezekano wa kumnunua mshambuliaji wa Tottenham Harry Kane, 29, kwani Spurs hawataki kumuuza nahodha huyo wa England, haswa kwa timu nyingine ya Ligi ya Premia. (Sky Sports)
Tottenham wanatazamiwa kuwasiliana na Brentford ili kujadili kuhusu ada ya kumnunua kipa wa Uhispania David Raya. Lakini Spurs na wawindaji wenzao Manchester United wanasita kulipa pauni milioni 40 ambazo Nyuki hao wanazitaka kwa mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 27. (Sky Sports)
Winga wa Crystal Palace Wilfried Zaha, 30, anatazamiwa kukataa ofa ya pauni milioni 30 kwa mwaka ili kujiunga na klabu ya Saudi Arabia Al-Nassr, huku Paris St-Germain na Marseille zikiwa na nia ya kumsajili mshambuliaji huyo wa Ivory Coast kwa uhamisho wa bila malipo msimu huu. . (Guardian)
Newcastle United wanatayarisha ofa ya kumnunua kiungo wa kati wa Wolfsburg Mjerumani Felix Nmecha, 22, ambaye anatarajiwa kugharimu takriban £15m, na pia wanamtazama kiungo wa kati wa Nice na Ufaransa Khephren Thuram, 22. (Telegraph - subscription required)
Kiungo wa kati wa Uholanzi Frenkie de Jong, ambaye alilengwa na Manchester United mwaka jana, anatarajia kuichezea Barcelona msimu ujao na mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 26 huenda akawa muhimu kwa mipango ya meneja Xavi. (Voetbal International, via Manchester Evening News)
Aston Villa wanatazamia kumleta mkurugenzi wa michezo wa Sevilla Monchi, ambaye alifanya kazi na meneja Unai Emery katika klabu hiyo ya Uhispania. (Express & Star)
BBC



