Mbeya City imefanikiwa kuibuka na ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya KMC katika mchezo wa kwanza wa play-off kuwania kusalia ligi kuu ya NBC
Sixtus Sabila na Mwaiposa walifunga mabao ya Mbeya City wakati bao la KMC lilifungwa na Abdul Hilal
Timu hizo zitarudiana tena jijini Dar es salaam katika mchezo wa pili utakaopigwa Ijumaa, Juni 16 katika uwanja wa Uhuru
KMC itahitaji ushindi wa angalau bao 1-0 ili kupindua meza wakati Mbeya City watahitaji ushindi au matokeo yoyote ya sare
Timu itakayopata ushindi katika matokeo ya jumla itabaki ligi kuu wakati timu itakayopoteza itacheza mechi nyingine ya play-off dhidi ya timu iliyoshinda mchezo wa play-off kupanda ligi kuu