PSG - Real Madrid - International

Mbappe aitega PSG

Joel JJ By Joel JJ
β€’
13 Jun 2023
Mbappe aitega PSG

Swali kubwa ambalo mpaka sasa halina majibu huko barani Ulaya ni kwamba wapi ataelekea mshambuliaji Kylian Mbappe kutoka Paris Saint Germain, badaa ya taarifa kuwa klabu hiyo inapanga kumuuza Mfaransa huyo msimu huu wa joto

Imeripotiwa kuwa hatua hiyo ni baada ya PSG kuhofia huenda ikampoteza bure mchezaji huyo kwakuwa mkataba wake umebaki mwaka mmoja huku akigoma kuongeza mkataba mwingine

Awali kulikuwa na taarifa ya tarehe ya mwisho ya Julai 31, 2023 kwa Mbappe, 24, kuwaambia PSG kama angebaki PSG hadi 2025

Baada ya mazungumzo miezi kadhaa, Mbappe alitoa barua kuwa hatofanya hivyo

Hata hivyo, wakati mabingwa hao wa Ufaransa wakijaribu kurekebisha sera yao ya ujenzi wa timu baada ya miaka mingi ya kununua wachezaji nyota bila mkakati madhubuti, PSG wameazimia kutomwachia Mbappe bure, huku klabu hiyo ikikerwa na barua hiyo kuvujishwa kwenye vyombo vya habari kabla

Real Madrid wanamtamani kwa muda mrefu Mfaransa huyo na alikataa kuhamia Bernabeu kusalia PSG mwaka jana

Kuondolewa kwa Karim Benzema kwenda Saudi Arabia kunamaanisha kuwa Real inahitaji mshambuliaji, ingawa ilifikiriwa kuwa Harry Kane wa Tottenham alikuwa kileleni mwa orodha yao

Mbappe, ambaye alijiunga na PSG mwaka 2017 kwa mkopo akitokea Monaco kabla ya uhamisho wa euro 180m, amefunga mabao 212 katika michezo 260

Ana mabao 38 katika mechi 68 alizoichezea Ufaransa, ikiwa ni pamoja na hat-trick katika fainali ya kombe la Dunia mwaka jana nchini Qatar, Ufaransa iliposhindwa na Argentina kwa mikwaju ya penalti

Mbappe alimaliza kama mfungaji bora wa Ligue 1 katika kila misimu mitano iliyopita na ameshinda mataji matano ya ligi katika misimu yake sita akiwa PSG.

More Stories

Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
9h ago
READ MORE β†’
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
9h ago
READ MORE β†’
Highlights : Azam Fc 0-2 Simba
Highlights : Azam Fc 0-2 Simba
9h ago
READ MORE β†’
Mizizima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
Mizizima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
13h ago
READ MORE β†’
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
16h ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
17h ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
17h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
18h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
19h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
20h ago
READ MORE β†’