Klabu ya Simba imetangaza kuachana na mtaalamu wa viungo Dk Fareed Cassim pamoja na aliyekuwa Kocha wa viungo Kelvin Mandla
Meneja wa Habari na Mawasiliano klabu ya Simba Ahmed Ally amesema ni mchakato wa maboresho ya benchi la ufundi ambapo pamoja nao, Kocha wa magolikipa Chlouha Zakaria hatakuwa sehemu ya kikosi cha Simba msimu ujao
Uongozi wa Simba umepania kurejea ubora wa Simba kuanzia kwenye benchi la ufundi ambalo ndio kama jiko




